Psalms 88:15-18


15 aTangu ujana wangu nimeteseka, nikakaribia kifo;
nimepatwa na hofu zako, nami nimekata tamaa.

16 bGhadhabu yako imepita juu yangu;
hofu zako zimeniangamiza.

17 cMchana kutwa zinanizunguka kama mafuriko;
zimenimeza kabisa.

18 dUmeniondolea marafiki na wapendwa wangu;
giza limekuwa ndilo rafiki yangu wa karibu kuliko wote.
Copyright information for SwhKC